Utangulizi
Moja ya somo Muhimu sana kwa mkristo anayetarajia kuingia mbinguni. Bila ubatizo wa kweli mtu hataweza kuingia katika ufalme wa MUNGU. Mtu asiyebatizwa katika ubatizo wa kweli hatambuliki katika kitabu cha uzima katika ufalme wa MUNGU.
Ubatizo ni Nini
Ubatizo kibiblia ni tendo takatifu lililoamriwa na MUNGU, linaloonyesha toba ya dhambi, kuokoka, na kuanza maisha mapya ndani ya KRISTO. Ni ishara ya nje inayoonyesha kile kilichotokea ndani ya moyo wa mtu.
Maana ya Ubatizo Kibiblia
Maana yake ya kwanza ni Kuzikwa na kufufuka pamoja na KRISTO, Biblia inasema;
Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama KRISTO alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.
- Unazikwa dhambi zako za zamani
- Unafufuka kuishi maisha mapya
- Ishara ya toba ya kweli
- Ubatizo unaambatana na kuacha dhambi
Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake YESU KRISTO, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha ROHO MTAKATIFU.
Hivyo ubatizo si kuoga tu, bali ni uamuzi wa kuacha maisha ya zamani.
Kuingia katika familia ya MUNGU. Ni ishara ya kuunganishwa na YESU KRISTO na kuwa sehemu ya mwili wake yaani kanisa.
Kufuata Mfano wa YESU KRISTO
YESU KRISTO mwenyewe alibatizwa. Hivyo kama sisi ni wanafunzi wake, na tunajifunza kwake, lazima na sisi tubatizwe. Maandiko yanasema,
13 Wakati huo YESU akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe.
14 Lakini Yohana alitaka kumzuia, akisema, Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?
15 YESU akajibu akamwambia, Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote. Basi akamkubali.
16 Naye YESU alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona ROHO wa MUNGU akishuka kama hua, akija juu yake;
17 na tazama, sauti kutoka mbinguni ikisema, Huyu ni Mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye,
Hivyo ubatizo ni ishara kwamba yeye anayefanya hivyo anamtii MUNGU kwa kufuata maelekezo yake. Maana Yesu alifanya hivyo kwa kutimiza na kufuata maelekezo kutoka kwa Baba.
Kubatizwa kwa Maji Mengi / Kuzamishwa
Neno "Ubatizo" linatokana na neno la Kigiriki BAPTIZO linalomaanisha "KUZAMISHA."
Hivyo ubatizo wa kibiblia unafanyika kwa kuzamishwa majini, si kunyunyiziwa. Hivyo tendo la ubatizo kwa usahihi linapaswa kufanyika kwa kuzamishwa ndani ya maji mengi.
Kwa maana imeandikwa
YESU akajibu, Amin, amin, nakuambia, Mtu asipozaliwa kwa maji na kwa ROHO, hawezi kuuingia ufalme wa MUNGU.
Na kule kuzamishwa kunamaana kubwa sana yaani kufa na kufufuka. Tunapozamishwa ni ishara ya kitendo cha kufa na tunapoibuka ni ishara ya kitendo cha kufufuka pamoja na KRISTO.
Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama KRISTO alivyofufuka katika wafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.
Kwa hiyo ubatizo usio sahihi utawapeleka wengi katika jehanamu ya moto. Tutajifunza kuhusu ubatizo wa jina la Baba, mwana na ROHO MTAKATIFU ni sahihi au sio sahihi kulingana na maandiko
Kwa maana imeandikwa
Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la baba, na Mwana, na ROHO MTAKATIFU;
Katika somo hili tujifunze ubatizo wa kweli kwa jina la BWANA YESU kwa kuangalia vipengele hivi;
- SIRI ILIYO JIFICHA KATIKA BABA, MWANA, ROHO MTAKATIFU
- JINSI MITUME WALIVYOBATIZA UBATIZO WA JINA LA YESU
I: Siri Iliyo Jificha Katika Baba, Mwana, ROHO MTAKATIFU
TUANGALIE KUHUSU BABA
Kwa kusudi la kuelewa maana ya Baba, mwana na ROHO mtakatifu. Tutaenda kuchambua kwa undani ili tuelewe zaidi na Katika kipengele hiki tutaona nafasi ya baba katika familia. MUNGU amemuweka baba kuwa kichwa cha familia. Familia au ngazi ya familia inafananishwa na utawala wa MUNGU na MUNGU mwenyewe ndiye mwanzilishi wa familia. Tuangalie katika biblia tuone jinsi nafasi au ofisi ya Baba imeelezwa.
Mambo 4 Yanayomhusu Baba Ndani ya Familia Yake Katika Biblia
- Mtawala, kichwa au mfalme
- Mlinzi wa familia
- Mtoaji
- Mweka nidhamu
1. Baba: Mtawala, kichwa au mfalme
Baba Ameitwa kiungu kuwa nabii, kuhani, na mfalme katika nyumba yake, ili kuifundisha familia yake kutoka kwa Neno la MUNGU, kudumisha familia yake katika njia ya haki ya MUNGU, na kutawala familia yake kulingana na mapenzi ya MUNGU.
Ukatokea kwa ajili ya wokovu wa watu wako, Kwa ajili ya wokovu wa masihi wako; Ukakiponda kichwa cha nyumba ya waovu, Ukiuweka wazi msingi hata mwambani.
Tena mtu mume mmoja wa kila kabila atakuwa pamoja nanyi; kila mmoja aliye kichwa cha nyumba ya baba zake. Na majina ya hao waume watakaosimama pamoja nanyi ni haya; Wa Reubeni; Elisuri mwana wa Shedeuri.
Enyi wake, watiini waume zenu kama kumtii BWANA wetu. Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama KRISTO naye ni kichwa cha Kanisa; naye ni mwokozi wa mwili. Lakini kama vile Kanisa limtiivyo KRISTO vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo.
Hapa tunaona baba katika familia amepewa na fasi ya kuwa mtawala na kuwa kiongozi katika familia.
2. Baba: Mlinzi wa Familia
Akina baba wapo ili kuilinda familia, baba anapoacha kuilinda familia ndipo adui upata nafasi ya kuivamia familia. Tuone Mfano wa Mfalme wa Wafilisti Akishi Aliposhambulia Familia ya Daudi
Ikawa, Daudi na watu wake walipokuwa wamefika Siklagi siku ya tatu, hao Waamaleki walikuwa wameshambulia Negebu, na Siklagi, nao wameupiga Siklagi, na kuuchoma moto; nao wamewachukua mateka wanawake waliokuwamo wakubwa kwa wadogo; hawakuwaua wo wote, ila wakawachukua, wakaenda zao. Basi Daudi na watu wake walipoufikilia mji, tazama, ulikuwa umechomwa moto; na wake zao, na watoto wao, waume kwa wake, wamechukuliwa mateka. Ndipo Daudi na watu waliokuwa pamoja naye wakainua sauti zao na kulia, hata walipokuwa hawana nguvu za kulia tena. Na hao wake wawili wa Daudi walikuwa wamechukuliwa mateka, Ahinoamu wa Yezreeli, na Abigaili, aliyekuwa mkewe Nabali, wa Karmeli.
Hapa Daudi alikuwa mlinzi na alipewa jukumu la kuilinda nyumba yake dhidi ya mashambulizi kutoka kwa adui
3. Baba: Mtoaji wa Familia
Baba mara nyingi ukaa nafasi ya mtoaji wa familia. Kujishughulisha na kazi ili kuilea familia yake na kutoa mahitaji mbalimbali kama vile malazi, mavazi, chakula, elimu, na huduma za afya.
Lakini mtu ye yote asiyewatunza walio wake, yaani, wale wa nyumbani mwake hasa, ameikana Imani, tena ni mbaya kuliko mtu asiyeamini.
4. Baba: Muweka Nidhamu
Ni kwa ajili ya kurudiwa mwastahimili; MUNGU awatendea kama wana; maana ni mwana yupi asiyerudiwa na babaye?
Nanyi, akina baba, msiwachokoze watoto wenu; bali waleeni katika adabu na maonyo ya BWANA.
Kwa Hiyo Katika Ulezi, MUNGU Anasimama Katika Nafasi ya Baba, Mfalme, Mtawala. MUNGU ameonyesha Ubaba Wake kwetu kwa njia ya moja kwa moja kwa kuumba vitu vyote na kuanzisha mwanadamu, na kwa kuweka agano na uzao wake. MUNGU pia anaonyesha Ubaba Wake kwa njia ya upatanishi.
tazama toka mbinguni, ukaone toka makao ya utukufu wako na fahari yako; uko wapi wivu wako, na uweza wako? shauku ya moyo wako, na huruma zako zimezuiliwa kwangu. Maana wewe ndiwe Baba yetu, ijapokuwa Ibrahimu hatujui, wala Israeli hatukiri; wewe, BWANA, ndiwe Baba yetu, mkombozi wetu tangu milele ndilo jina lako.
Katika andiko hili MUNGU anaitwa BABA YETU
Siku zile nyumba ya Yuda watakwenda pamoja na nyumba ya Israeli, nao watakuja pamoja, kutoka nchi ya kaskazini, mpaka nchi ile niliyowapa baba zenu iwe urithi wao. Lakini mimi nalisema, Nitawezaje kukuweka pamoja na watoto, na kukupa nchi ipendezayo, urithi ulio mwema wa mataifa? Nami nikasema, Mtaniita, Baba yangu, wala hamtageuka na kuacha kunifuata.
Hapa tunaona MUNGU anataka tumwite Baba kwa sababu yeye ndiye anatupa urithi wa baraka zetu
Je! Sisi sote hatuna Baba mmoja? MUNGU aliyetuumba siye mmoja tu? Basi, mbona kila mmoja wetu anamtenda ndugu yake mambo ya hiana, tukilinajisi agano la baba zetu.
Hapa tunaona kuwa kwa sababu ya uumbaji, sisi ni Watoto wa MUNGU na yeye ni Baba yetu
Basi ikiwa ninyi, mlio waovu, mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamwombao?
Katika maombi tunayofanya kama wanadamu tunapaswa kutambua sisi ni wana wa MUNGU na MUNGU ni Baba Yetu.
wakamwambia, Angalia, wewe umekuwa mzee, na wanao hawaendi katika njia zako; basi, tufanyie mfalme atuamue, mfano wa mataifa yote. Lakini neno hilo likawa baya machoni pa Samweli, waliposema, Tupe mfalme atuamue. Naye Samweli akamwomba BWANA. BWANA akamwambia Samweli, Isikilize sauti ya watu hawa katika kila neno watakalokuambia; kwa maana hawakukukataa wewe, bali wamenikataa mimi, ili nisiwe mfalme juu yao.
Maandiko yanaonesha Dhahiri kuwa watu wanamkataa MUNGU asiwe mfalme juu yao na kuwatawala. Badala yake walitaka utawala wa wanadamu ili kujiongoza wenyewe.
TUANGALIE KUHUSU MWANA
Katika Ukombozi, MUNGU anasimama kama Mwana
Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, MUNGU mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa BWANA wa majeshi ndio utakaotenda hayo.
Hapa tunaona mwana mwenye sifa zote za MUNGU kabisa. Kwa hiyo katika ukombozi MUNGU hujifunua kama mwana ambaye ni YESU KRISTO
Katika Utawala, MUNGU Hujifunua kama Bwana
Katika maandiko BWANA ni YESU KRISTO.
Katika mwaka ule aliokufa mfalme Uzia nalimwona BWANA ameketi katika kiti cha enzi, kilicho juu sana na kuinuliwa sana, na pindo za vazi lake zikalijaza hekalu. Juu yake walisimama maserafi; kila mmoja alikuwa na mabawa sita; kwa mawili alifunika uso wake, na kwa mawili alifunika miguu yake, na kwa mawili aliruka. Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni BWANA wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake.
Hapa tunaona nabii isaya anamwona BWANA katika kiti chake cha enzi kama mtawala
BWANA wa majeshi ndiye mtakayemtakasa; na awe yeye hofu yenu, na awe yeye utisho wenu. Naye atakuwa ni mahali patakatifu; bali ni jiwe la kujikwaza na mwamba wa kujikwaa kwa nyumba za Israeli zote mbili, na mtego na tanzi kwa wenyeji wa Yerusalemu.
Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye KRISTO YESU mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe hekalu takatifu katika BWANA
Hapa andiko linaonesha YESU KRISTO ndiye BWANA.
kwamba uilinde amri hii pasipo mawaa, pasipo lawama, hata kufunuliwa kwake BWANA wetu YESU KRISTO; ambako yeye kwa majira yake atakudhihirisha, yeye aliyehimidiwa, Mwenye uweza peke yake, Mfalme wa wafalme, BWANA wa mabwana; ambaye yeye peke yake hapatikani na mauti, amekaa katika nuru isiyoweza kukaribiwa; wala hakuna mwanadamu aliyemwona, wala awezaye kumwona. Heshima na uweza una yeye hata milele. Amina.
YESU akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.
ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya MUNGU, na ahadi zake; ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka KRISTO kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, MUNGU, mwenye kuhimidiwa milele. Amina.
Lakini wewe je! Mbona wamhukumu ndugu yako? Au wewe je! Mbona wamdharau ndugu yako? Kwa maana sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha MUNGU. Kwa kuwa imeandikwa, Kama niishivyo, anena BWANA, kila goti litapigwa mbele zangu; Na kila ulimi utamkiri MUNGU. Basi ni hivyo, kila mtu miongoni mwetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za MUNGU.
ili kwa jina la YESU kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa MUNGU Baba.
Wala tusimjaribu BWANA, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka.
Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya KRISTO YESU; ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya MUNGU, naye hakuona kule kuwa sawa na MUNGU kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. MUNGU alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.
Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, asema BWANA MUNGU, aliyeko na aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi. Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na subira ya YESU KRISTO, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la MUNGU, na ushuhuda wa YESU. Nalikuwa katika ROHO, siku ya BWANA; nikasikia sauti kuu nyuma yangu, kama sauti ya baragumu, ikisema, Haya uyaonayo uyaandike katika chuo, ukayapeleke kwa hayo makanisa saba: Efeso, na Smirna, na Pergamo, na Thiatira, na Sardi, na Filadelfia, na Laodikia. Nikageuka niione ile sauti iliyosema nami. Na nilipogeuka, niliona vinara vya taa saba vya dhahabu; na katikati ya vile vinara nikaona mtu mfano wa Mwanadamu, amevaa vazi lililofika miguuni, na kufungwa mshipi wa dhahabu matitini. Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho yake kama mwali wa moto; na miguu yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti yake kama sauti ya maji mengi. Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake. Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.
TUANGALIE KUHUSU ROHO MTAKATIFU
Katika Utendaji au Uumbaji MUNGU Ujifunua kama ROHO MTAKATIFU
ROHO wa MUNGU ameniumba, na pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
Hapa ROHO MTAKATIFU anatajwa katika eneo la uumbaji. Tuangalie katika utendaji wa karama, huduma katika kanisa
Basi pana tofauti za karama; bali ROHO ni yeye yule. Tena pana tofauti za huduma, na BWANA ni yeye yule. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali MUNGU ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa ROHO kwa kufaidiana. Maana mtu mmoja kwa ROHO apewa neno la hekima; na mwingine neno la maarifa, apendavyo ROHO yeye yule; mwingine imani katika ROHO yeye yule; na mwingine karama za kuponya katika ROHO yule mmoja; na mwingine matendo ya miujiza; na mwingine unabii; na mwingine kupambanua roho; mwingine aina za lugha; na mwingine tafsiri za lugha; lakini kazi hizi zote huzitenda ROHO huyo mmoja, yeye yule, akimgawia kila mtu peke yake kama apendavyo yeye. Maana kama vile mwili ni mmoja, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule, navyo ni vingi, ni mwili mmoja; vivyo hivyo na KRISTO.
Maandiko yanasema kazi zote hizi huzifanya ROHO MTAKATIFU
ROHO MTAKATIFU NI MUNGU
Petro akasema, Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo ROHO MTAKATIFU, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja? Kilipokuwa kwako, hakikuwa mali yako? Na kilipokuwa kimekwisha kuuzwa, thamani yake haikuwa katika uwezo wako? Ilikuwaje hata ukaweka neno hili moyoni mwako? Hukumwambia uongo mwanadamu, bali MUNGU.
Hapa petro anamtambulisha na kumwelezea ROHO MTAKATIFU kuwa ni MUNGU mwenyewe.
Lakini ikiwa ROHO wa MUNGU anakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na ROHO wa KRISTO, huyo si wake. Na KRISTO akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu i hai, kwa sababu ya haki.
Katika andiko hili tunaona kuwa ROHO MTAKATIFU anatajwa kama ROHO wa KRISTO na ROHO Wa MUNGU.
Kwa hiyo BABA, MWANA, ROHO MTAKATIFU huwa ni ofisi au nafasi ambazo MUNGU huwa anatumia kujifunua kwa wanadamu. Hivi ni vyeo vya MUNGU kwa wanadamu na hatupaswi kubatiza kwa vyeo au nafasi za MUNGU.
II: Jinsi Mitume Walivyobatiza Ubatizo wa Jina la YESU
Maandiko yanaeleza wazi kuwa kanisa limejengwa katika misingi ya mitume na manabii. Manabii na mitume wa biblia wanatuma mwongozo sahihi wa jinsi ya kutumika mbele za MUNGU.
Imeandikwa
Mmejengwa juu ya msingi wa mitume na manabii, naye KRISTO YESU mwenyewe ni jiwe kuu la pembeni. Katika yeye jengo lote linaungamanishwa vema na kukua hata liwe hekalu takatifu katika BWANA. Katika yeye ninyi nanyi mnajengwa pamoja kuwa maskani ya MUNGU katika ROHO.
Tunapaswa kuwafuata mitume kama kielelezo sahihi cha jinsi ya kubatiza watu kwa sababu:
1. Mitume Walielewa kwa Ufunuo Jina Halisi la Wokovu
YESU KRISTO alisema:
Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;
Lakini mitume walibatiza kwa jina la YESU kwa sababu:
- Walitambua kwamba "jina" ni moja (umoja), si majina matatu
- Jina hilo lililofunuliwa ni YESU KRISTO
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo
2. Mitume Walifanya kwa Vitendo (Mfano Halisi)
Kila mahali walipobatiza, walitumia jina la YESU:
Matendo 2:38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake YESU KRISTO, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha ROHO MTAKATIFU
Matendo 8:16 kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake BWANA YESU. (Walibatizwa kwa jina la YESU)
Matendo 10:48 Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake YESU KRISTO. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha. (Kornelio na nyumba yake)
Matendo 19:5 Waliposikia haya wakabatizwa kwa jina la BWANA YESU. (Wanafunzi wa Efeso)
Hakuna mahali mitume walibatiza kwa maneno mengine tofauti.
3. Waliongozwa na ROHO MTAKATIFU, Si Akili Zao
Mitume hawakukosea, kwa sababu: Walijazwa ROHO MTAKATIFU
Hata ilipotimia siku ya Pentekoste walikuwako wote mahali pamoja. Kukaja ghafula toka mbinguni uvumi kama uvumi wa upepo wa nguvu ukienda kasi, ukaijaza nyumba yote waliyokuwa wameketi. Kukawatokea ndimi zilizogawanyikana, kama ndimi za moto uliowakalia kila mmoja wao. Wote wakajazwa ROHO MTAKATIFU, wakaanza kusema kwa lugha nyingine, kama ROHO alivyowajalia kutamka.
Lakini yeye atakapokuja, huyo ROHO wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake.
Hivyo walichofanya si bahati mbaya, bali ni mapenzi ya MUNGU yaliyofunuliwa.
4. Jina la YESU Lina Mamlaka Yote
Biblia inasema:
ili kwa jina la YESU kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
Hivyo ubatizo kwa jina la YESU, Unabeba mamlaka kamili, Unahusisha wokovu moja kwa moja
5. Mitume Ndio Msingi wa Mafundisho Sahihi
Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.
Hivyo
- Tukifuata wao, tunafuata ukweli
- Tukiacha wao, tunaingia katika mapokeo ya wanadamu
Mitume Walivoamuru na Kutenda Kuhusu Ubatizo wa Jina la YESU
1. Mtume Paulo Aliwaagiza Wakristo wa Kolosai
Mtume paulo aliwaagiza wakristo wa kolosai kuwa kila wafanyalo kwa tendo au neno wafanye kwa jina la YESU. Imeandikwa
NA KILA MFANYALO, KWA NENO AU KWA TENDO, FANYENI YOTE KATIKA JINA LA BWANA YESU, MKIMSHUKURU MUNGU BABA KWA YEYE.
Ubatizo ni tendo linapaswa lifanyike katika jina la YESU.
2. Mtume Petro Aliagiza Watu Wabatizwe Katika Jina la YESU KRISTO
mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake YESU KRISTO, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha ROHO MTAKATIFU.
Hapa watu walibatizwa kwa jina la YESU KRISTO na sio nafasi au vyeo vya MUNGU kwa wanadamu anapojifunua kwako.
3. Mtume Petro Aliamuru Akida Kornelio Abatizwe kwa Jina YESU
Akaamuru wabatizwe kwa Jina lake Yesu Kristo. Ndipo wakamsihi azidi kukaa siku kadha wa kadha.
4. Mtume Filipo Aliwabatiza Watu kwa Jina la YESU KRISTO
Imeandikwa
12 Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa MUNGU, na jina lake YESU KRISTO, wakabatizwa, wanaume na wanawake.
13 Na yeye Simoni mwenyewe aliamini akabatizwa, akashikamana na Filipo; akashangaa alipoziona ishara na miujiza mikubwa inayotendeka.
14 Na mitume waliokuwako Yerusalemu, waliposikia ya kwamba Samaria imelikubali neno la MUNGU, wakawapelekea Petro na Yohana;
15 ambao waliposhuka, wakawaombea wampokee ROHO MTAKATIFU;
16 kwa maana bado hajawashukia hata mmoja wao, ila wamebatizwa tu kwa jina lake BWANA YESU.
5. Towashi Alibatizwa Katika Jina la YESU KRISTO na Mtume Filipo
Imeandikwa
36 Wakawa wakiendelea njiani, wakafika mahali penye maji; yule towashi akasema, Tazama, maji haya; ni nini kinachonizuia nisibatizwe?
37 Filipo akasema, Ukiamini kwa moyo wako wote, inawezekana. Akajibu, akanena, Naamini ya kwamba YESU KRISTO ndiye Mwana wa MUNGU.
38 Akaamuru lile gari lisimame; wakatelemka wote wawili majini, Filipo na yule towashi; naye akambatiza.
39 Kisha, walipopanda kutoka majini, ROHO wa BWANA akamnyakua Filipo, yule towashi asimwone tena; basi alikwenda zake akifurahi.
Kabla ya ubatizo, towashi alipewa msingi wa kuliamini jina la YESU KRISTO na akabatizwa jina hilo la BWANA YESU
Mwisho, mtu anapaswa kubatizwa kwa jina la YESU KRISTO na sio Vyeo au ofisi za MUNGU yaani Baba, mwana na ROHO MTAKATIFU.
6. Mtume Petro Anasema Hakuna Wokovu Nje ya Jina la YESU
10 jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la YESU KRISTO wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na MUNGU akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu.
11 Yeye ndiye jiwe lile lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni.
12 Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.
Hapa tunaona maandiko yanasema; bila jina la YESU KRISTO hakuna wokovu kwa mwanadamu yeyote chini ya mbingu.
Ubatizo si Desturi tu
Ni muhimu kukumbuka kwamba ubatizo si desturi tu, bali ni agano takatifu kati ya mtu na MUNGU. Biblia inatuonyesha wazi kupitia mitume kwamba ubatizo wa kweli ulifanyika kwa jina la YESU KRISTO na kwa kuzamishwa majini, baada ya mtu kutubu na kuamini.
Kama Ulibatizwa:
- Kwa kunyunyiziwa maji,
- Au bila ufahamu wa toba na imani binafsi,
- Au bila kutumia jina la YESU KRISTO,
basi ni wakati wa kutafakari upya na kuchukua hatua sahihi ya imani.
Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake YESU KRISTO, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha ROHO MTAKATIFU.
Hii inaonyesha wazi kuwa ubatizo wa kweli:
Unaanza na toba
Unafanyika kwa jina la YESU KRISTO.
Unahusishwa na msamaha wa dhambi
Hata katika Matendo 19:1–5, wale waliokuwa wamebatizwa awali walipofundishwa ukweli, walibatizwa tena kwa jina la YESU KRISTO.
Ikawa, Apolo alipokuwa Korintho, Paulo, akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko; akawauliza, Je! Mlipokea ROHO MTAKATIFU mlipoamini? Wakamjibu, La, hata kusikia kwamba kuna ROHO MTAKATIFU hatukusikia. Akawauliza, Basi mlibatizwa kwa ubatizo gani? Wakasema, Kwa ubatizo wa Yohana. Paulo akasema, Yohana alibatiza kwa ubatizo wa toba, akiwaambia watu wamwamini yeye atakayekuja nyuma yake, yaani, YESU. Waliposikia haya wakabatizwa kwa jina la BWANA YESU.
Hivyo basi, kama bado hujabatizwa kwa njia hii ya kibiblia, au ulibatizwa kwa kunyunyizwa, usiogope kuchukua hatua ya Imani.
MUNGU anakuita leo:
Njoo kwa toba ya kweli,
Pokea ubatizo sahihi,
Na anza maisha mapya ndani ya KRISTO.
Usikawie; wokovu ni sasa
Pastor Obed Joseph Katunzi