Wito wa Huduma

Mtumishi wa Mungu Walter Mrisha alipokea wito wa kumtumikia Mungu kipindi alipookoka tuu, mnamo mwaka 2018. Baada ya kubatizwa, alianza kuhubiri Injili mitaani na kuombea wagonjwa. Hii ilikuwa katika mkoa wa Dar es salaam. Baada ya kufanya huduma hiyo miezi kadhaa, alisafiri kuelekea mkoani Kilimanjaro ili kwenda kujijenga vizuri kiroho.

Januari 2019, alianza mafunzo ya huduma ya Mungu katika Chuo cha Mafunzo na Uongozi Usangi, kilichopo huko Mwanga-Kilimanjaro na kuhitimu mwaka 2021.

Baada ya kuhitimu, alianza kufanya huduma ya mikutano ya Injili, semina makanisani, uinjilisti wa mtaani na nyumba kwa nyumba, maombi na maombezi katika maeneo mbalimbali ya Tanzania ikiwemo Dar-es-salaam, Tabora, Dodoma, Singida, Arusha, Tanga na Kilimanjaro.

Kwasasa, anamtumikia Mungu kupitia huduma ya Wanafunzi wa Yesu, ambayo iko chini ya kanisa la Revelation and Testimony Church of God (Kanisa Takatifu la Mungu), lenye makao yake makuu Tegeta, Dar-es-salaam.

Ubatizo Sahihi ni Huu

Ubatizo Kibiblia Utangulizi Moja ya somo Muhimu sana kwa mkristo anayetarajia...